Gavana Waititu aliaibishwa wakati wa sherehe za Mashujaa Dei

February 2024 ยท 2 minute read

- Waititu aliamshwa kwenye eneo la VIPs wakati wa sherehe za Mashujaa Mombasa

- Waititu anakabiliwa na kesi kuhusu uporaji wa mali ya kaunti ya Kiambu

- Rais Kenyatta hataki kukaribiwa na kiongozi yeyote ambaye anahusishwa na kashfa za ufisadi

Gavana wa Kiambu Ferdinand Waititu anazidi kujipata mabaya katika safari yake ya kisiasa baada ya kuhusishwa na kashfa ambapo serikali ya Kiambu ilipoteza shilingi milioni 588.

Aidha siku ya Mashujaa Dei ya mwaka huu ambapo sherehe zilifanyika kaunti ya Mombasa itabakia mojawapo wa siku mbaya zaidi kisiasa.

Habari Nyingine: Hatimaye Size 8 azima fununu na kukiri kuwa ni mjamzito

Kulingana na gazeti la Nation la Jumanne, Oktoba 22, Waititu alikatazwa kuketi pamoja na viongozi wengine mashuhuri katika eneo la VIPs.

Inaarifiwa Waititu alifika katika eneo la sherehe hizo na kuchukua nafasi katika eneo la VIPs kabla ya maafisa wa usalama kufika hapo na kumtaka aamke mara moja.

Bila kubishana, Waititu alijifanya anazungumza kwa siku na kuamka kabla ya kuingia mitini.

Habari Nyingine: Moto wazidi kuwaka nyumbani kwa Raila, Ida Odinga adaiwa kutoa taarifa za uongo

Duru zinaarifu Waititu baadaye aliondoka kutoka kwenye sherehe hizo kichinichini na hakuonekana tena.

Kulingana na maafisa waliokuwa wakihusika na kuandaa sherehe hizo za mashujaa, walisema kulikuwa na maagizo makali kutoka Ikulu kuwa viongozi wowote walio na kesi za ufisadi ama wanaochunguzwa wasikaribie Rais Uhuru Kenyatta.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjZ31zhZZmnpqukaOubsPAoquirKVirq21wKKZoquYrK5uw8CkmK2hXayubr%2FHnqmeoJVix6J5zJqqoa2alq5usMSiZaGsnaE%3D